NAIBU WAZIRI WA WIZARA YA MAWASILIANO ,SAYANSI NA TEKNOLOJIA ATEMBELEA TCRA

Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia January Makamba akipokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Profesa John Nkoma, wakati alipotembelea Makao Makuu.

TCRA 4

Prof. Nkoma speaking with the press after the visit of Minister of Communications from malawi

TAMKO LA SERIKALI KUHUSU UHAMAJI KUTOKA MFUMO WA UTANGAZAJI WA ANALOJIA KWENDA DIJITALI

Mabadiliko katika mfumo wa utangazaji kutoka mfumo wa analojia kwenda katika mfumo wa dijitali ni utaratibu ambao unaendelea ulimwenguni kote. Mabadiliko haya yanatokana na makubaliano ya nchi wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa lenye dhamana ya masuala ya mawasiliano yaani International Telecommucations Union yaliyofanyika mwaka 2005 huko Geneva, Uswisi. Makubaliano ya nchi wanachama ni kuzima kabisa matangazo katika mfumo wa analojia na kutumia mfumo wa utangazaji wa dijitali ifikapo tarehe 17 Juni 2015.

Ili kuhakikisha mabadiliko haya yanafanyika kwa ufanisi, tija na pia kutoa muda wa kutosha wa kutekeleza mabadiliko haya, mwaka 2005 Serikali ilianza mchakato wa uhamaji kutoka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda dijitali ambao ulihusisha wadau wote, wakiwemo wamiliki wa vyombo vya habari na vituo vya utangazaji wa televisheni, hatua kwa hatua, hadi kuridhia ratiba nzima ya uzimaji wa mitambo ya analojia. Kwa kifupi mchakato wa uhamaji ulipitia hatua zifuatazo:

Moshi, Arusha kuingia dijitali

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema, inatarajia kuzima mitambo ya kurusha matangazo ya televisheni ya mfumo wa analojia katika Mji wa Moshi na Jiji la Arusha Machi 31 mwaka huu.
Kuzimwa kwa maeneo hayo kunafikisha jumla ya mikoa sita ambayo ni Dar es Salaam, Tanga, Dodoma na Mwanza  ambayo tayari inapokea matangazo ya televisheni kwa njia ya dijitali na kubaki Mkoa wa Mbeya utakaozimwa Aprili 30, mwaka huu.
Meneja  Mawasiliano wa Mamlaka hiyo, Inocent Mungi akizungumza katika kipindi cha Jambo Tanzania cha Shirika la Utangazaji TBC1  juzi, aliwataka wadau kushirikiana na TCRA ili kuondoa changamoto zilizopo zinazotokana na mfumo huo.

TCRA KANDA YA MASHARIKI YATOA SEMINA YA MAJUKUMU YA MAMLAKA HIYO KATIKA WILAYA YA MAFIA


Hawa Sulemani akijisomea moja ya vipeperushi vya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania baada ya kugawiwa katika semina ya Majukumu ya Mawasiliano Kanda ya Mashariki iliyofanyika katika Wilaya ya Mafia kwa kuwashirikisha viongozi mbalimbali wa wilaya hiyo.
Baadhi ya Washiriki wa Semina ya Majukumu ya Mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Mashariki iliyofanyika katika Wilaya ya Mafia wakijisomea majaridi yenye ujumbe mbalimbali na Kazi za Mamlaka hiyo. Baaada ya kugawiwa na Mhasibu wa TCRA BW.Patrice Lumumba.
Washiriki wa semina ya Majukumu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Kanda ya Mashariki iliyofanyika katika Wilaya ya Mafia wakishiriki katika zoezi la kutambua simu bandia.wakati walipokuwa wakionzwa na Afisa Utumishi Mkuu Esuvatie Masinga (hayupo pichani)
Mhandisi wa Masafa wa Mamlaka ya Mawssiliano Kanda ya Mashariki Stella Bunyenza akitoa mada ya Ukuaji wa Teknolojia wakati wa Semina ya Majukumu ya Mamlaka ya Mawsiliano Tanzania (TCRA)Kanda ya Mashariki iliyofanyika katika Wilaya ya Mafia.
Mhasibu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Kanda ya Mashariki Patrice Lumumba akitoa maada ya Mfumo wa Anuani za Makazi na Posti Kodi wakati wa Semina ya Majukumu ya Mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Mashariki iliyofanyika Wilayani Mafia.
Mkuu wa Wilaya ya Mfia Sauda Mtondoo akimkabidhi Prudence Nyombi zawadi ya King’amuzi cha Star timu baada ya kujishindia kutokana na kujibu swali aliloulizwa juu ya matumizi ya Mawasiliano, wakati wa Semina ya Majukumu ya Mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Mashariki iliyofanyika Wilayani Mafia.katikati ni Mkurugenzi wa Watumiaji na Watoa Huduma za Mawasiliano Dk. Raymond Mfungahema akishuhudia.
Mkurugenzi wa Watumiaji na Watoa Huduma za Mawasiliano Dk. Raymond Mfungahema akimkabidhi zawadi ya simu aina ya Nokia Mkuu wa Wilaya ya Mafia Bi,Sauda Mtondoo wakati wa Semina ya Majukumu ya Mamlaka ya Mawsiliano Tanzania (TCRA)Kanda ya Mashariki iliyofanyika katika Wilaya ya Mafia.

TCRA Yatwaa Tuzo ya Ubingwa Sekta za Fedha nchini.


Mstahiki Meya wa Ilala, Mhe. Jerry Slaa, akimkabidhi cheti cha Ushindi wa Jumla, Kaimu Meneja Mawasiliano wa TCRA, Semu Mwakyanjala
*******
Na Pascal Mayalla.
Mamlaka ya Mawasiliano Nchini, TCRA, imeshinda Tuzo ya Tasisi Bora ya Mawasiliano ya Kifedha nchini, baada ya kuibuka na ushindi wa jumla kwenye maonyesho ya Seta ya Fedha nchini, yaliyomalika jana, kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar Es Salaam.

Ushindi huo wa TCRA, umepatikana kufuatia makampuni , Asasi na Tasisi za kifedha nchini, zilizoshiriki katika maonysho hayo, kupimwa jinsi huduma zake zinavyosaidia ukuaji wa sekta ya fedha nchini, ambapo TCRA imeibuka na ushindi huo kufuatia kutoa vibali na number maalum kwa makampuni ya simu na taasisi za kifedha nchini kutumia number number hizo kwa huduma za kifedha, ziitwazo SIM Banking, kulikopekea Watanzania wengi zaidi kufikiwa na huduma za kifedha kwa njia ya rahisi zaidi .

Ushindi wa pili umetwaliwa na kampuni ya simu za mkoni ya Vodacom kupitia huduma yake ya M-Pesa ikielezewa hii ndio huduma ya pesa iliyosambaa nchini kote na kutumiwa na mamilioni ya Watanzania kama mkombozi wao katika huduma za kifedha.

Kwa upande wa mabenki, Benki ya CRDB ndio imeshinda kama benki kiongozi katika maonyesho hayo kwa kuwa ndio benki pekee hapa nchini, iliyoshiriki maonyesho hayo kwa kishindo kikubwa kwa kuwakilishwa na benki yenyewe ya CRDB PLC na kampuni yake tanzu ya CRDB Microfinance LTD iliyoelezwa kuwa ndio benki pekee iliuyowafikia wajasiliamali wadodo wadogo wa vijini kuliko benki nyingine yoyote.

RAIS KIKWETE AMKARIBISHA WAZIRI MKUU WA DENMARK IKULU JIJINI DAR LEO

Mamia ya wananchi wakijiandaa kumlaki Waziri Mkuu wa Denmark Mhe Helle Thorning-Shmidt kupitia lango la Mashariki la Ikulu Dar es salaam leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Waziri Mkuu wa Denmark Mhe Helle Thorning-Shmidt  Ikulu Dar es salaam leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mgeni wake Waziri Mkuu wa Denmark Mhe Helle Thorning-Shmidt wakiingia Ikulu huku wakishangiliwa.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika maongezi ya faragha na Waziri Mkuu wa Denmark Mhe Helle Thorning-Shmidt leo Ikulu.